Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mollel, Waitara, Silinde waneemeka CCM

Thursday , 29th Oct , 2020

Katika uchaguzi huu Chama Cha Mapinduzi (CCM) miongoni mwa wagombea wake wa ubunge nchi nzima pia walikuwemo wagombea watatu  wa ubunge ambao walitokea Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika miaka ya mwanzoni na wengine dakika za lala salama bunge likiwa linaelekea kuvunjwa,

Pichani ni Wabunge wateule kwa tiketi ya CCM, Kushoto ni Godwin Mollel (Siha), Mwita Waitara (Tarime Vijijini), Kulia ni David Silinde (Tunduma)

 kuvunjwa ambao ni Mwita Waitara, Godwin Mollel na David Silinde.

Kwa upande wake David Silinde hapo awali alikuwa Mbunge wa jimbo la Mbozi Mjini tangu 2010  kwa tiketi ya CHADEMA baada ya kuhamia CCM na kupitishwa kuwania ubunge aligombea jimbo la Tunduma ambapo ameibuka msindi kwa kura 43,276 dhidi ya mshindani wake Frank Mwakajoka wa CHADEMA aliyepata kura 12,433.

Aidha kwa upande wa Dkt Godwin Mollel yeye aliingia Bungeni mwaka 2015 na mwaka 2017 alikihama chama chake ''CHADEMA'' na kutimkia CCM, Disemba 2017 akiwa sehemu ya kuunga mkono juhudi zilizokuwa zikifanywa na serikali ya awamu ya tano, katika uchaguzi mdogo uliofanyika Februari 2008 Mollel aliibuka mshindi kwa kupata kura  25,611 huku Elvis Mosi wa CHADEMA akipata kura 5,905 na katika uchaguzi Mkuu huu amepata kura 22,172, akifuatiwa na Elvis Mossi wa CHADEMA aliyepata kura 8614.

Kwa upande wake Mwita Waitara alichaguliwa kuliongoza Jimbo la Ukonga kwa tiketi ya CHADEMA mwaka 2015, alijiuzulu na kujiunga na CCM mwezi Julai 2018 na baada ya siku 4 tangu kuapishwa kwake bungeni Waitara aliteuliwa na Rais John Magufuli  tarehe 10 Novemba 2018 kuwa Naibu waziri wa TAMISEMI katika mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya