Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kisa cha mwalimu aliyekutwa 'Guest' na mtoto

Friday , 25th Sep , 2020

TAKUKURU mkoa wa Mbeya, inamshikilia Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nyeregete iliyoko wilayani Mbarali, Adelhard Mjingo, (44), kwa tuhuma za kuomba rushwa ya ngono kwa mwanafunzi wake wa darasa la saba mwenye umri wa miaka 14 kwa ahadi ya kuwa angemsaidia kufaulu mitihani.

Ofisi ya TAKUKURU mkoa wa Mbeya

Taarifa hiyo imetolewa leo Septemba 25, 2020 na mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Julieth Matechi, na kusema kuwa mwalimu huyo alinaswa na makachero wa TAKUKURU mnamo Septemba 23 mwaka huu akiwa na mwanafunzi huyo kwenye moja ya nyumba za kulala wageni.

Matechi amesema, siku ya tukio mwalimu huyo aliaga shuleni kuwa anaenda kwenye semina ya chanjo katika Mji wa Rujewa wilayani humo na aliondoka pamoja na walimu wenzake lakini alipofika kwenye ukumbi aliandikisha jina na kuomba udhuru kisha akaondoka na kwamba wakati mwalimu huyo anaondoka shuleni alimtaka mwanafunzi wake aende nyumbani kubadili nguo.

"Mwalimu huyo alichukua chumba kwenye nyumba ya kulala wageni iitwayo Executive iliyopo Rujewa na kisha akamtuma dereva bodaboda kwenda kumchukua binti huyo na alipofika naye mwalimu alimpokea na kuingia naye chumbani, baada ya kuingia na mwanafunzi huyo chumbani alitoka na kwenda kumnunulia chipsi na soda kisha akaingia tena chumbani kwa ajili ya kutimiza azma yake", amesema mkuu wa TAKUKURU.

Aidha Matechi ameongeza kuwa wakati mwalimu huyo akijiandaa kutekeleza uhalifu huo, makachero wa TAKUKURU waliokuwa wanafuatilia tukio hilo waliingia na kumuweka chini ya ulinzi mwalimu huyo, na kwa sasa taasisi hiyo inaendelea na uchunguzi na utakapokamilika atachukuliwa hatua za kisheria.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani