Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Janeth asimulia alivyovumilia ukatili kwa miaka 17

Friday , 18th Sep , 2020

Janeth Masawala ameiasa jamii kuhakikisha inamjengea mtoto wa kike uwezo wa kujihami na kuweza kujua namna ya kukabiliana na ukatili ikiwemo vipigo ndani ya ndoa, vitakavyoleta athari kimwili na hata kiafya, kama ambavyo yeye aliathirika na kuwa na kansa ya koo sababu ya vipigo.

Janeth Masawala, mwanamke aliyepitia ukatili wa vipigo kwa mume wake

Janeth ametoa kauli hiyo hii leo Septemba 18, 2020, kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio wakati akisimulia namna alivyoweza kuvumilia vipigo ndani ya ndoa yake kwa kipindi cha miaka 17.

"Tulifunga ndoa mwaka 1998 baada ya wiki tu vipigo vikaanza, nilikuwa napigwa mpaka nazimia kuna kipindi alinipiga kidogo mimba ya mwanangu wa kwanza ikataka kuharibika, unakuta ana visababu vingi mfano mbona mboga ina mafuta", amesema Janeth.

Aidha Janeth akielezea namna alivyopata saratani amesema kuwa, "Ndoa ilinisababishia nipate vipigo na kutokana na vile vipigo kwa muda mrefu ikapelekea goita kuvimba na baadaye kugundulika nina saratani, madhara ya vipigo ni mengi wako wanaopata presha lakini mimi imenipelekea kupata saratani", amesimulia Janeth.

"Nakumbuka tukio jingine, nilipigwa halafu nikafungiwa ndani wiki nzima bila msaada na nilivyokuja kuzinduka nikawa kama chizi, na kwa vile sikuwa sawa nikajikuta nimekunywa pombe kali nikazima kwa siku tatu tena", amesimulia Janeth.

Janeth Masawala kwa sasa ni mwanaharakati wa kutetea haki za wanawake, ambapo amewaomba wanawake wanaopitia ukatili wasijifungie ndani na badala yake watoke kutafuta msaada.
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani