Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Janeth asimulia alivyovumilia ukatili kwa miaka 17

Friday , 18th Sep , 2020

Janeth Masawala ameiasa jamii kuhakikisha inamjengea mtoto wa kike uwezo wa kujihami na kuweza kujua namna ya kukabiliana na ukatili ikiwemo vipigo ndani ya ndoa, vitakavyoleta athari kimwili na hata kiafya, kama ambavyo yeye aliathirika na kuwa na kansa ya koo sababu ya vipigo.

Janeth Masawala, mwanamke aliyepitia ukatili wa vipigo kwa mume wake

Janeth ametoa kauli hiyo hii leo Septemba 18, 2020, kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio wakati akisimulia namna alivyoweza kuvumilia vipigo ndani ya ndoa yake kwa kipindi cha miaka 17.

"Tulifunga ndoa mwaka 1998 baada ya wiki tu vipigo vikaanza, nilikuwa napigwa mpaka nazimia kuna kipindi alinipiga kidogo mimba ya mwanangu wa kwanza ikataka kuharibika, unakuta ana visababu vingi mfano mbona mboga ina mafuta", amesema Janeth.

Aidha Janeth akielezea namna alivyopata saratani amesema kuwa, "Ndoa ilinisababishia nipate vipigo na kutokana na vile vipigo kwa muda mrefu ikapelekea goita kuvimba na baadaye kugundulika nina saratani, madhara ya vipigo ni mengi wako wanaopata presha lakini mimi imenipelekea kupata saratani", amesimulia Janeth.

"Nakumbuka tukio jingine, nilipigwa halafu nikafungiwa ndani wiki nzima bila msaada na nilivyokuja kuzinduka nikawa kama chizi, na kwa vile sikuwa sawa nikajikuta nimekunywa pombe kali nikazima kwa siku tatu tena", amesimulia Janeth.

Janeth Masawala kwa sasa ni mwanaharakati wa kutetea haki za wanawake, ambapo amewaomba wanawake wanaopitia ukatili wasijifungie ndani na badala yake watoke kutafuta msaada.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya