
Nyota wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Ulimwengu.
Ulimwengu amechelewa kujiunga na Taifa Stars kutokana na klabu yake, TP Mazembe ya DRC Congo kumuomba abaki kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu nchi humo. Mchezaji huyo ameingia nchini leo, jijini Dar es salaam na moja kwa moja kuingia kambini.
Taifa Stars sasa inamsubiri mshambuliaji na Nahodha, Mbwana Samatta wa KRC Genk ya Ubelgiji pekee, ambaye naye klabu yake ilimuomba abaki kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa mchujo wa kuwania kucheza Europa League msimu ujao.
Samatta na Ulimwengu, wote wameziongoza klabu zao kushinda mwishoni mwa wiki, Genk ikiilaza 5-1 Sporting Charleroi na kufuzu Europa League na Mazembe ikiichapa 2-0 AS Vita katika Ligi ya DRC Congo.