Tuesday , 1st Apr , 2014

Shirikisho la soka Tanzania TFF limesema kuwa taarifa za kuwepo kwa vitendo ama mchezo mchafu katika baadhi ya michezo ya ligi kuu ya soka Tanzania bara inayoelekea ukingoni wamezisikia.

TFF wamesema, wao kama shirikisho wanazifanyia kazi kwa kuanza kuchunguza ukweli wa tuhuma hizo

Afisa habari wa TFF Boniface Wambura amesema kuwa na katika kuhakikisha wanadhibiti hali ya upangaji matokeo hasa katika michezo ya mwisho ya ligi hiyo wameamua kupanga michezo yote ifanyike kwa siku na mda mmoja japo hilo linaweza lisiwe tiba ya moja kwa moja.

Pia takaye bainika kupanga matokeo kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria na timu yake pia kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni na sheria za soka