
Katibu Chama cha Soka Wilaya ya Mufindi Festo Kilupamwambu amesema, wana nafasi kubwa kwa kutumia fursa katika mzunguko kuweza kupanda daraja kwani katika mzunguko wa kwanza timu hiyo ya Kurugenzi inashika nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 14 huku anayeongoza akiwa na pointi 16.
Kilupamwambu amesema, wanahitaji kuwa na idadi kubwa ya timu za ligi kuu kwani mpaka sasa ukanda wa kusini ndiyo unaotoa vipaji vingi hivyo wanahitaji kuhakikisha wanakuwa na timu zaidi ya tano shiriki za ligi kuu tofauti na hivi sasa ambapo zipo timu tatu ambazo ni Tanzania Prisons, Mbeya City na Majimaji.