
Nadal ambaye ameshinda taji lake la 11 la Michuano ya wazi ya Ufaransa Jumapili iliyopita, amesema sababu kuu ya kujitoa kwenye michuano hiyo ni kupata muda wa kujiandaa na michuano ya Wimbledon inayoanza Julai 2.
"Nimeongea na madaktari wangu wamenishauri nipumzike ili niweze kuweka sawa mwili wangu kabla ya kuingia kwenye michuano ya Wimbledon'', amesema Nadal mwenye miaka 32.
Aidha Nadal amewaomba msamaha mashabiki wake pamoja na waandaaji wa michuano hiyo ambao walikuwa wamejiandaa kumuona nguli huyo wa tenisi duniani.