Friday , 4th Apr , 2014

Ule mpambano wa kimataifa wa ngumi za kulipwa uliokua ufanyike kesho baina ya bondia mtanzania Francis Miyeyusho na bondia mphilipino Ronald Pontillas umesogezwa mbele hadi aprili 12 mwaka huu

Mratibu wa mpambano huo Musa Kova amesema kuwa pamoja na mambo yaliyojitokeza mpaka pambano hilo limesogezwa mbele lakini kama waandaaji wamejipanga kuhakikisha mambo yanakwenda sawa.

Kubwa zaidi siku hiyo watanzania wataua ndege wawili kwa jiwe moja kwani pia mtanzania mwingine Francis Cheka atashuka uliongoni kuvaaan na bondia bingwa wa Iran.