Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Cannavaro atetea Yanga kufungwa

Sunday , 13th Aug , 2017

Beki kisiki wa kati na nahodha wa timu ya Yanga Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema kujifunga kwa beki mpya wa timu hiyo hapo jana Abdallah Hajji ‘Ninja’  ni moja ya matukio ya mchezo na isitafsriwe kwamba beki huyo ni uchochoro au ana uwezo mdogo.

Cannavaro amesema 'Ninja' ni beki chipukizi mwenye uwezo mkubwa na kinachomkumba sasa hivi ni presha ya timu hiyo kutokana na kwanza ndiyo amesajiliwa na hakuwahi kucheza timu kubwa kama Yanga hivyo ana mambo ya kujifunza kwa wakati huu inabidi apewe muda ili azoee mazingira na baadaye matunda yake yataonekana.

Beki Hajji ‘Ninja aliyejifunga 

Cannavaro amesema hayo ikiwa ni siku moja tangu timu hiyo hapo jana jioni ipoteze mchezo wa kirafiki baada ya kufungwa bao 1-0 na Ruvu Shooting Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam ambapo beki Hajji ‘Ninja’ alimfunga kwa kichwa cha mkizi kipa wake, Ramadhan Awam Kabwili dakika ya 22 wakati akijaribu kuokoa krosi ya Shalla Juma kutoka upande wa kushoto wa Uwanja na kuipatia bao pekee la ushindi Ruvu Shooting.

Huo ulikuwa mchezo wa pili wa kujipima nguvu kwa Yanga inayofundishwa na kocha Mzambia, George Lwandamina baada ya Jumamosi iliyopita kushinda 3-2 dhidi yas Singida United Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Na baada ya matokeo hayo, Yanga SC imeondoka hii leo jijini Dar es Salaam mapema kwenda Zanzibar ambako usiku huu watamenyana na Mlandege Uwanja wa Amaan katika mchezo mwingine wa kirafiki.

Mapema kesho Jumatatu Yanga watakwenda kisiwani Pemba kuweka kambi ya kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba Agosti 23 Uwanja wa Taifa. 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani