Mfungaji bora wa muda wote wa NBA LeBron James usku wa jana Oktoba 22, 2024 aliweka rekodi nyingine  kwenye ligi ya kikapu Marekani maarufu NBA. King aliweka rekodi ya  kuchangia uwanja na mwanawe LeBron ‘Bronny’ James Jr mwenye umri wa miaka 20 kwenye mchezo uliozikutanisha  LA Lakers dhidi ya Minnesota TimberWolves  waliposhinda vikapu 110 kwa vikapu 103.

23 Oct . 2024

Nyota wa Real Madrid ya Hispania Vinicius Junior usiku wa jana Oktoba 22, 2024 aliushangaza ulimwengu wa Soka baada ya kuonyesha kiwango bora kwenye mchezo wa ligi ya Mabingwa barani Ulaya dhidi ya Borrusia Dortmund uwanja wa Santiago Bernabeu. Vini alifunga magoli matatu na kuiongoza Madrid kupata ushindi wa goli 5-2.

23 Oct . 2024

Klabu ya Coastal Union ya Tanga  imemtangaza Juma Mwambusi kuwa kocha mkuu wa timu hiyo baada ya kumfuta kazi aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo David Ouma raia wa Kenya mwezi Agosti 2024. Kikosi hiko cha Wagosi wa Kaya kilikuwa chini ya Joseph Lazarao ambaye alikaimu kwa muda kipindi ambacho timu hiyo ilipokuwa inatafuta Mwalimu Mkuu.

23 Oct . 2024

Pichani ni msanii Ruger na Bob Marley

23 Oct . 2024

Nahodha wa zamani wa Uruguay na Mchezaji wa klabu ya Manchester United ya England atashiriki mashindano ya Tennis yatakayofanyika Uruguay Montevideo. Forlan ana umri wa miaka 45 atashirikiana na Federico Coria kwenye michezo ya wawili kwa wawili.

22 Oct . 2024

Vikundi vya ulinzi shirikishi

22 Oct . 2024

Aishi Manula mara ya mwisho kuitumikia timu ya taifa ya Tanzania ilikua mwezi Machi 2024.Kumekua na mjadala mkubwa kwa Wapenzi na Wadau wa soka nchini Tanzania kuhusiana na nafasi ya Golikipa huyo wa timu ya Simba kwenye kikosi cha Stars. Manula hana Wakati mzuri kwenye klabu yake ya Simba ameondolewa kwenye nafasi yake ya kuwa golikipa namba moja baada ya kuumia kwa muda mrefu na aliporejea uwanjani kwenye mchezo wa Dabi ya Kariakoo alifanya makosa yaliyochangia kupoteza mchezo kwa goli 5-1.

22 Oct . 2024

Pichani Ni Esma Platnumz na Yammi

22 Oct . 2024