Jumatatu , 19th Jan , 2026

Producer Zest sound killer amefunguka sababu za kutaka kuona video ya wimbo wa Wasanii harmonize na ibraahz Friendzone, Zest ameeleza hayo kwenye mahojiano na Friday Night Live

Pichani Zest Harmonize na Ibraah

"Sijajua kama wameshashoot ila kiukweli Friendzone ni bonge moja la ngoma nazopenda kuzisikiliza,idea na production ni kali sana kwahiyo natamani nione video'' Ameandika Zest sound killer

"Naamini Harmonize Ibraah ni mdogo wake kama (Ibraah) amemkosea anaweza tu akamsamehe na mambo yakaendelea,napenda kuona wakiwa wanafanya kazi pamoja''Ameandika Zest sound killer