Friday , 28th Nov , 2014

Polisi nchini Uganda wameomba ushauri wa wataalamu wa picha kubaini iwapo picha za utupu za mwanamuziki Desire Lusinda zilizosambazwa mitandaoni ni zake halisi ama zimefanyiwa ujanja.

msanii wa muziki wa Uganda Desire Luzinda

Hatua hiyo ya polisi ni sehemu ya uchunguzi mpana wa tukio hilo, lililozua mjadala mkubwa nchini Uganda, na kuvuka mipaka ya nchi hiyo kutokana na umaarufu wa Desire Luzinda.

Tangu kusambazwa kwa picha hizo kumekuwa na makundi mawili moja linamlaumu msanii Desire kwa mienendo michafu, huku wengine wakimtetea na kusema msanii huyo ni mhanga wa tukio hilo.