
msanii wa muziki wa Uganda Mun G akiwa na mchumba wake Clara
Harusi ya msanii huyu inatarajiwa kuwa tukio jingine kubwa katika ulimwengu wa burudani Uganda ambapo mpaka sasa mashabiki wa msanii huyu wanasubiri kwa hamu kutangazwa kwa tarehe rasmi ya tukio la harusi ya staa huyu.
Mun G ambaye jina lake halisi ni Emmanuel Matovu pamoja na mchumba wake ambaye anafahamika kwa jina Clara, wamekuwa wakiishi pamoja tangu mwanzoni mwa mwaka huu, na sasa msanii huyu ameamua kumaliza mwaka kwa kurasimisha uhusiano wake huo kwa mujibu wa taratibu za kiimani na kiutamaduni.
