Wednesday , 27th Jan , 2016

Kutoka Yamoto Band, msanii mpya anayeishika bendi hiyo kwa upande wa unenguaji licha ya ulemavu wa mguu alionao, Chiba ametoa wito kwa watu wenye ulemavu kujituma kiubunifu katika kufanya kazi, akiamini kuwa kuonesha kazi nzuri kunazaa mafanikio.

Chiba

Chiba ametolea mfano wa yeye binafsi kujituma na kufanya kazi ambayo asilimia kubwa ya mashabiki wanaifurahia sasa, ambayo imetokana na jitihada zake binafsi akiwa sasa na nafasi ya kupanda katika majukwaa makubwa kuonyesha kipaji chake.

Chiba kupitia kazi yake ya unenguaji muda mrefu bila kuchoka jukwaani, amekuwa ni moja kati ya wasanii ambao majina yao yanaendelea kushika chati kwa kiasi kikubwa, akitarajiwa kufanya makubwa mwaka huu kwa upande wa unenguaji.