Friday , 15th Jan , 2016

Afisa anayesimamia masuala ya haki za kibinaadamu katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa ana ushahidi kwamba vikosi vya usalama vya Burundi viliwabaka wanawake vilipokuwa vikitafuta nyumba za wafuasi wa upinzani

Zeid Ra'ad al Hussein amesema kuwa unyanyasaji huo ulitokea baada ya shambulio la waasi katikati ya mwezi Disemba dhidi ya kambi tatu za kijeshi.

''Ishara zote ikiwemo kuongezeka kwa mgogoro wa kikabila zinaonyesha ushahidi'',alisema katika taarifa.

Burundi ipo katika hali ya sintofahamu kutokana na Rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunzinza kujiongezea muda wa kuendelea kuongoza nchi hiyo.

Chanzo BBC