Sunday , 10th Jun , 2018

Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, amewataka watanzania kuwa na uvumilivu wa masuala ya kidini ili nchi iendelee kuwa na amani, utulivu na maendeleo.

Ndugai ametoa wito huo katika Kata ya Pahi wilayani Kondoa mkoani Dodoma, alipokuwa akizungumza wakati wa mashindano ya kuhifadhi Qur'an yaliyowashirikisha zaidi ya watoto na vijana 40 kutoka maeneo mbalimbali ya nchi.

Spika Ndugai ameeleza kuwa umoja na mshikamano uliopo hapa nchini ni matokeo ya viongozi wa dini mbalimbali hapa nchini kuendelea kuhubiri amani na utulivu na kuitaka jamii na viongozi hao kuiendeleza kazi hiyo

"Waziri wa Mambo ya Ndani anafanya kazi ya kuangalia shughulia za kidini ndani ya  nchi yetu zinandelea kwa amani kati ya dhehebu na dhehebu, endeleeni kuhubiri amani kila siku. Kazi iliyoifanywa na nyie Masheikh ni kubwa mno kwani kama amani mmeihubiri na tayari watanzania wameshaishika.  Watanzania wanauvumilivu wa kipekee sasa inabidi kuhubiri uvumilivu wa kidini" Ndugai.