Sunday , 20th Nov , 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 20 Novemba, 2016 amemteua Bw. Charles E. Kichere kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Rais Magufuli

Bw. Charles E. Kichere anajaza nafasi ya Naibu Kamishna Mkuu wa TRA iliyokuwa wazi kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, imesema kuwa uteuzi huu umeanza mara moja.

Kichere amewahi kuwa Mkuu wa Idara ya Fedha na Mhasibu Mkuu katika Wakala wa barabara Tanzania, (TANROADS)