
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Njombe Eluminata Mwenda.
Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Njombe Eluminata Mwenda wakati akiwasilisha taarifa ya utekeleza wa miradi kwa kipindi ambacho halmashauri ilikabidhiwa kwa watendaji huku madiwani wakiwa katika uchaguzi.
Taarifa hiyo iliyosomwa mbele ya madiwani wapya baada ya kuapishwa kwao Mwenda amesema kuwa kwa kipindi ambacho halmashauri haikuwa na madiwani wamepokea asilimia tano ya bajeti nzima ya utekelezaji wa maendeleo.
Aidha mwenda amesema kuwa halmashauri ya mji wa Njombe imefanikiwa kuhakikisha kuwa imebadilisha baadhi ya sheria ndogondogo za halmashauri hiyo ili kuhakikisha zinaboreshwa na kufanya kazi bila kuwapo kwa vikwazo.