Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Majaliwa aagiza wakulima wakopeshwe

Tuesday , 23rd May , 2017

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka taasisi za fedha ikiwemo Benki ya Maendeleo ya  Kilimo Tanzania (TADB) kuwekeza zaidi katika kukopesha wakulima waweze kununua matrekta yatakayowasaidia kulima kilimo cha kisasa na kuinuka kiuchumi.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipotembelea kiwanda cha kuunganisha matrekta URSUS-TAMCO, Kibaha mkoani Pwani.

Majaliwa amesema hayo leo alipokuwa akitembelea eneo la viwanda la TAMCO lililoko katika kitovu cha mji katika halmashauri ya mji wa Kibaha na kujionea hatua za awali za uunganishaji matrekta na zana zake unaofanywa kwa kushirikiana na wataalamu kutoka kampuni ya URSUS ya Poland.

Amesema ameridhishwa na uwepo wa viwanda katika mkoa wa Pwani na kuwa ni fursa kwa wananchi wa mkoa huo hususani wakulima hivyo endapo watakopeshwa matrekta wataweza kuongeza tija katika kilimo na kuinuka kiuchumi hatimaye  kuleta matokeo  chanya.

Mkurugenzi Mwendeshaji  wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Mlingi Mkucha amesema hadi sasa tayari yameunganishwa matrekta yapatayo 92 na kuwa kwa awamu ya kwanza ya mradi huo unatarajia kuunganisha jumla ya matrekta 2400.

Amesema mradi huo umegharimu kiasi cha dola milioni 55 ikiwa ni pamoja na ujenzi wa kiwanda na kufunga mitambo na vifaa vya kuunganisha matrekta.

Naye Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage amesema nchi ina viwanda vikubwa vipatavyo 393 na kati ya hivyo 84 viko mkoani Pwani, hivyo alizitaka halmashauri kuepuka kutoza tozo kubwa la viwanja ili kuwavutia wawekezaji, waweze kumudu gharama na kuendelea kuwekeza zaidi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu