Monday , 20th Jun , 2016

Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria Nchini Inatarajiwa Kutumia Zaidi ya Shillingi Billioni Hamsini Kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo Cha Kutafuta na Kuokoa Watu Wanaopata Ajali Katika Ziwa Hilo Jijini Mwanza.

Meli ya MV Bukoba iliyozama Ziwa Victoria mwaka 1996 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 800

Kituo Hicho Ambacho Pia Kitasaidia Kutoa Huduma ya Uokozi Kwa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki Kitaanza Kujengwa Kati ya Mwezi wa Tisa na Mwezi wa Kumi na Mbili Mwaka Huu Kwa Makubaliano na Benki ya Maendeleo ya Africa.

Mtaalamu wa Masuala ya Usafiri na Usalama wa Vyombo Vya Majini ,Mhandisi Gerson Fumbuka, Amesema Kwa Kiasi Kikubwa Ajali za Majini Zimekuwa Zikiongezeka Ukubwa Kutokana na Kukosekana Kwa Vifaa Vya Uokozi Kama Vile Maboya na Wataalamu na Hivyo Kupitia Kituo Hicho Wanatarajia Kitasaidia Kupunguza Majanga Hayo