Tuesday , 18th Mar , 2014

Madereva wa boda boda na bajaji katika jiji la Dar es salaam nchini Tanzania wameiomba serikali kuwaruhusu kuendelea kuchukua abiria na kuwafikisha kati kati ya jiji kutokana na kuanza kushuka kwa vipato vyao.

Wakizungumza na East Africa Radio leo katika Vijana hao wameishauri serikali kwamba ni vema wakaondoa vituo vya boda boda na bajaji kati kati ya jiji badala ya kuwazuia kufika kutokana na wengi wa abiria wao wanatoka na kwenda kati kati ya jiji.

Wamesema iwapo serikali itaendelea na uamuzi wake wataathirika katika kupata kipato kwa kuwa wengi wa waendesha boda boda na bajaji ni wale waliokabidhiwa na watu binafsi ambao wanahitaja kupeleka hesabu za fedha kwa mujibu wa makubaliano.