Thursday , 23rd Jun , 2016

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha muswada wa fedha wa mwaka 2016 unaolenga kufanyia marekebisho sheria 16 zinazohusu masuala ya Fedha ,Kodi, Ushuru ,Tozo na Mawasiliano kwa ajili ya kuidhinisha bajeti ya serikali kwa mwaka 2016/17

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Phillip Mpango

Muswada huo unalenga kutunga sheria ya fedha kwa ajili ya kuweka, kurekebisha, kupunguza pamoja na kufuta kodi, ushuru ada na tozo mbalimbali kwa lengo la kuboresha ukusanyaji wa kodi.

Akiwasilisha Muswada huo leo Bungeni mjini Dodoma, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Phillip Mpango amesema katika marekebisho hayo, ni pamoja na kupunguza misamaha ya kodi isiyo na tija, kupunguza kiwango cha chini cha kutoza kodi ya mapato yatokanayo na ajira, kuiwezesha Mamlaka ya Mapato Tanzania kukusanya kodi ya majengo badala ya halmashauri na kuweka sharti kwa kampuni za simu kujiorodhesha katika Soko la Hisa ili watanzania wanunue hisa.

Wakizungumza na EATV baadhi ya wabunge wamekuwa na maoni mbalimbali kuhusiana na muswada huo kama ifuatavyo

Dkt Philip Mpango
Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini
Rose Tweve, Mbunge Viti Maalum CCM