Koffi kupamba harusi ya Bona Mugabe
Msanii wa muziki Koffi Olomide leo hii atatumbuiza huko nchini Zimbabwe katika sherehe ya harusi ya binti wa rais wa nchi hiyo, Bona Mugabe anayefunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi, Simba Chikore ambaye anafanya shughuli za urubani wa ndege.