Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta, akisalimiana na kiongozi wa dini ya Kiislamu nchini Tanzania, Sheikh Mkuu Mufti Shaaban Simba jijini Dar es Salaam jana.
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Samwel Sitta ameeleza kuwa amefanya mazungumzo na viongozi wakuu wa dini ili kutoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo ambayo yalikuwa yakifikishwa kwa viongozi hao.