Usahili wa mwisho Dance 100% wakamilika kwa mtiti

Makundi matano yaliyoingia robo fainali leo yakiwa katika picha ya pamoja.

Usahili wa mwisho wa Dance 100% 2015, umekamilishwa katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam, muamko mkubwa wa makundi yapatayo 28 kutoka ndani na nnje ya mkoa yakiongezea ushindani na burudani zaidi katika michuano hiyo kuelekea kupata makundi mengine 5 yatakayoshinda uchaguzi.

Katika michuano ya leo, Wazawa Crew, The Best, Quality Boys, Majokeri na kundi la wasichana la Cute Babies waliweza kuwashawishi majaji na kuweza kujivunia alama nyingi zaidi zilizowawezesha kushinda nafasi ya kuingia robo Fainali ya Dance 100% 2015.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS