RPC Arusha atoa ofa kwa walevi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Jonathan Shana, katika kusherehekea sikukuu ya Eid El Fitri, ametoa ofa kwa mtu yeyote atakayelewa kupita kiwango ahakikishe anawasiliana na Jeshi hilo, kwa ajili ya kulichukua gari lake na kulihifadhi na atapaswa kulifuata pale ulevi utakapomwisha.