Rais wa Kenya William Ruto
Hayo ameyabainisha hii leo Septemba 4, 2023, wakati akihutubia kwenye uzinduzi rasmi wa Kongamano la Mabadiliko ya Tabianchi Afrika 2023 katika Ukumbi wa KICC, Nairobi, kiongozi wa nchi alisema.
"Miezi isiyo mbali kutoka sasa, tutaondoa hitaji la visa kwa Waafrika wanaotembelea Kenya, sio haki unapotembelea nyumbani hadi uwe na viza," amesema Rais Ruto
Hatua hiyo ya kufungua mipaka ya Kenya kwa nchi zote za Bara Afrika, inawiana na mikakati ya Afrika Mashariki ambapo raia wa ukanda huu hawahitaji kuwa na visa kuzuru nchi yoyote Afrika Mashariki.
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imeundwa na mataifa 7, yanayojumuisha; Burundi, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Uganda na Tanzania.
Kongamano la Mabadiliko ya Tabianchi Afrika 2023, limehudhuriwa na zaidi ya Maraisi 20 kutoka Barani, na viongozi mashuhuri ulimwenguni, kampuni na mashirika yanayotetea uhifadhi wa mazingira.