Jumanne , 18th Jul , 2023

Idadi ya waliofariki dunia katika msitu wa Shakahola nchini Kenya sasa hivi imefikia 419 baada ya mili 16 kufukuliwa katika makaburi mengine hii leo Julai 18, 2023.

Picha za kutoka msitu wa Shakahola

Mratibu wa usalama Kaunti ya Mombasa Rhoda Onyacha amesema kwamba maafisa wanaoshughulikia ufukuaji wa miili ya Shakahola waliko wafuasi wa mhubiri Paul Makenzi, wanaoendeleza ibada ya kufunga hadi kufa sasa imefikia 419.

Aidha watu waliookolewa mpaka sasa ni 95, na washirikishi wa Makenzi 37 wanashikiliwa na vyombo vya usalama na shughuli ya kutafuta makaburi na kuyafukua bado inaendelea.