Pikipiki zilizokabidhhiwa kwa Jeshi la Polisi Iringa
Akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano Mkuu wa mkoa wa iringa Halima Dendego amewapongeza wadau kutoka sekta binafsi kwa kutoa vifaa vya usafiri kama sehemu ya kupanua wigo wa mapambano dhidi ya vitendo vya uhalifu pamoja na kurudisha fadhila kwa jamii
Kwa upande wao baadhi ya wadau waliofanikisha zoezi hilo ikiwa ni pamoja na kampuni ya Asas, East African Bornwood, Yisen International Investment, wamesema kuwa lengo la kutoa mchango huo ni kuongeza ufanisi wa kazi zinazofanywa na jeshi hilo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa ACP Allan Bukumbi, amesema kuwa kwa sasa wanaendelea na zoezi la utoaji mafunzo kwa askari watakaotumia pikipiki hizo ili kutambua matumizi sahihi na utunzaji wa vyombo hivyo vya moto