Jumatano , 14th Jun , 2023

Mtu mmoja amefariki  dunia huku 8 wakijeruhiwa katika ajali ya kontena  la lori lililoanguka katika kona ya Yombo mwisho wa Lami  wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam jana Juni 13/2023

Wakazi wa eneo hilo wameomba serikali kuliangalia eneo hilo kutokana na kukosa matuta na alama za kusaidia kuitakbuliaha kuonesha  kona hiyo.

Wakizungumzia ajali hiyo iliyotokea jana mchana  eneo la Yombo mwisho wa Lami  mwenyekiti wa  serikali ya mtaa wa Machimbo Rahim Maridadi pamoja na baadhi ya wananchi wa eneo la Yombo wamesema tukio hilo limetokea jana

mchana ambapo lori hilo likiwa katika hali ya mwendokasi lilimshinda dereva na kudondosha kontena ambalo lilipelekea  majeruhi na kifo cha mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Bahati Christandus .

Mganga mfawadhi wa hospitali ya Temeke Dkt.  Joseph Kimaro  amethibitisha kupokea majeruhi  wanne na mwili mmoja ambapo majeruhi hao akiwemo mtoto mdogo ambaye ni mtoto wa marehemu Bahati aliyeokolewa na mama yake wakiwa wanaendelea vyema .

Nyumbani kwa marehemu Bahati Christandus baahi ya majirani na ndugu wa marehemu wameendelea kuombeleza huku msemaji wa  familia Gabriel Mtole amethibitisha mtoto aliyejeruhiwa kuwa ni  mtoto wa marehemu na aliumia baada ya mama yake  kumrusha ili amuokoe kufuatia ajali hiyo.