Alhamisi , 14th Apr , 2022

Afrika Kusini imemshutumu Balozi wa Ukraine nchini humo kwa kufanya mambo yasiyo ya kidiplomasia
Balozi huyo anasemakana kutumia mtandao wake wa Twitter kuomba kuonana na Rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa, jambo ambalo Mamlaka za Afrika kusini zimesema ni kutafuta taharuki kwa umma.

Ameeleza anataka kuonana na  Cyril Ramaphosa kuzungumzia juu ya Vita vinavyowndelea nchini mwake huko mashariki mwa ulaya.

Balozi  Liubov Abravitova amesema kuwa amelazimika kutumia mtandao wa Twitter kuomba kuonana na Rais baada ya mmalaka za nchi hiyo kumnyima kuonananae mara kadhaaa alipoomba wakutane.

Kupitia mtandao wa Twitter Balozi huyo amesema “Toka Urusi ivamie nchi yangu, sijaruhusiwa kabisa kuonana na Rais ama mawaziri wa Afrika Kusini, Watu wangu wanashambuliwa Sana na majeshi ya Russia" Balozi  Abravitova ameandika.

Lakini Clayson Monyela, mmoja wa maafisa wa ngazi za juu ndani ya wizara ya mambo ya nje  nchini Afrika Kusini, amekana shutuma hizo na kusema kuwa Balozi huyo alishapewa nafasi ya kuonana na baadhi ya maafisa wa serikali.