
Dkt. Albina Chuwa, Mtakwimu Mkuu wa Serikali
Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt Albina Chuwa amewambia waandishi wa habari kuwa kuna matapeli wamejitokeza na kusajili tovuti isiyo rasmi, huku baadhi ya watu wakiwa wameanza kujisajili kupitia tovuti hiyo batili.
Aidha Dkt Albina Chuwa amesema kwamba kazi ya kuwapata watumishi wa sense itasimamiwa na kamati za sense za mikoa ambazo wenyeviti wake ni Wakuu wa Mikoa husika.