Mbwa na Polisi waliozuia kongamano la CHADEMA Mwanza
Hapo jana Julai 20, 2021, Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel, alipiga marufuku mikusanyiko isiyo ya lazima katika mkoa huo kwa ajili ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa hatari wa Corona.
Hadi EATV inaondoka katika eneo hilo jitihada za kumpata Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Ramadhan Ng’anzi, ziligonga mwamba baada ya kupigiwa simu mara kadhaa na kutopokea, lakini hivi karibuni RPC huyo alisema hatoruhusu kufanyika kwa mikutano isiyokuwa na vibali.