
Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Kalambo
Amesema kuwa tabia hiyo ilianza kwa watendaji wachache kutumia fedha wanazokusanya hali iliyopelekea na watendaji wengine kuiga tabia hiyo na matokeo yake kuwa desturi kwa watendaji hao kutumia fedha za makusanyo huku ikisomeka kuwa ni wadaiwa (defaulters) jambo ambalo Mwenyekiti huyo analipinga na kusema watendaji hao sio wadaiwa bali ni wezi wa fedha za halmashauri na hivyo wachukuliwe hatua kama wezi.
“Imekuwa Shida, kuna watendaji ambao sasa hivi wanaona kuwa TAKUKURU nako ni kama nyumbani, na sisi njia nyingine ambayo tunayo, nguvu yetu tuliyonayo ni ya kuwafukuza tu na kuwapeleka mahakamani, kwasababu hatuna namna, tumewapeleka kwenye vyombo ambavyo ndio tunavitegemea, zimefanya kazi yake kwa nguvu zote, tumekwenda hivyo lakini…” Alisema.
Aliongeza kuwa kuna baadhi ya watendaji wadaiwa ambao wameshajiandikisha ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kalambo ili ifikapo tarehe 30.05.2020 wawe wamemaliza kulipa fedha hizo na kushauri kuwa watendaji hao wasisubiriwe hadi ifike tarehe hiyo, kwani kuna watendaji ambao madeni yao ni makubwa na hivyo hawataweza kulipa fedha hizo kwa pamoja na kuitaka ofisi hiyo kuweka utaratibu wa watendaji hao kulipa kidogokigdogo.
Hadi kufikia tarehe 23.04.2020 halmashauri za Mkoa wa Rukwa zinadai zaidi ya shilingi milioni 928 za makusanyo ambayo hayajawasilishwa benki kutoka kwa watendaji, huku halmashauri ya Wilaya ya kalambo ikiwa ya pili kwa kudai ambapo watendaji wake wanadaiwa shilingi 260,496,059 na madiwani wa halmashauri hiyo wakidai zaidi ya shilingi milioni 80.