Ijumaa , 28th Feb , 2020

Mwanamitandao aliyejipatia umaarufu kufuatia unywaji wa bia Piere Likwidi, amewataka Watanzania  waendelee kutumia vinywaji vya Kampuni ya TBL  kwa sababu inalipa na imepewa tuzo kutoka Ulaya.

Picha ya Piere Likwidi

Piere Likwidi amesema hayo  wakati wa onyesho wa tuzo hiyo  ya Kimataifa ya Kizibo Cha Dhahabu (IGCA), iliyopewa kampuni ya TBL kutoka Ulaya ambayo ina kilo 16.01 za dhahabu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.

"Hii ni dhahabu tupu ambayo TBL wameshinda zawadi hii kutoka Ulaya ambao wametuona sisi tunafaa na wanywaji wazuri wa gambe, halafu tunyweni  gambe linalipa jamani kwanza linakimea kizuri kunywa na wewe ufaidi kama mimi ninavyofaidi" amesema Piere Likwidi.

Onyesho la zawadi ya tuzo hiyo ya dhahabu kutoka TBL, litaendelea kupitishwa mitaani na leo watakuwa maeneo ya Karume na Buguruni  wilayani Ilala, jijini Dar Es Salaam.