Picha ya kimbunga kilichotokea Arusha.
Akizungumza na EATV & EA Radio Digital, leo Oktoba 2, 2019, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha ACP Koka Moita, amesema kuwa mtu huyo anadaiwa kuzama majira ya saa 9:00 jioni siku ya Oktoba 1, lakini licha ya jitihada za uokozi kufanyika hawakuweza kumpata.
''Wilaya ya Arumeru katika mbuga ya Arusha ndani ya ziwa Momella, kulikuwa na watalii wawili waliokuwa wamekodisha mitumbwi, upepo ulivyokuja ulileta dhoruba na mitumbwi ikaanza kuyumba, lakini mtumbwi mmoja uliweza kutoka salama lakini yule nahodha wa mtumbwi wa pili ambaye ni mtanzania alizama na siku ya jana hatukufanikiwa kumpata'', amesema Kamanda Moita.
Kamanda Moita ameongeza kuwa juhudi za kumuokoa mtu huyo zinaendelea kwa kushirikiana na Jeshi la polisi, TANAPA pamoja na Jeshi la Zimamoto na uokoaji.