
Spika huyo wa Bunge anatarajiwa kuapishwa mapema siku ya Alhamis, ambapo Waziri Mkuu wa nchi ya Tunisia ametangaza siku saba za maombolezo.
Rais Essebsi amefariki akiwa na umri wa miaka 92 na kwamba amefariki akiwa hajamaliza muhula wake wa Urais.
Inaaminika kuwa Essebsi ndiye Rais mkongwe zaidi duniani ambapo aliingia madarakani baada ya kushinda uchaguzi huru wa kwanza wa nchi hiyo, kufuatia vuguvugu la maandamano katika mataifa ya kiarabu.