Beno Kakolanya
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF leo Disemba 3, 2018 imeelea kuwa kamati hiyo haijaketi hivi karibuni na wala hakuna shauri la Kakolanya lililowasilishwa katika kamati hiyo.
''Kamati ya Sheria na Hadhi za wachezaji haijakaa kupitia suala hilo kwahiyo taarifa hizo ni za uongo na zinasambazwa na watu wachache kwa maslahi yao'', imeeleza taarifa hiyo.
Kakolanya amekuwa na sintofahamu na klabu yake ya Yanga kutokana na kutoonekana kwenye kikosi hicho tangu alipotoka nchini Lesotho alipokuwa na timu ya tiafa kwenye mchezo wa kufuzu AFCON.
Taarifa iliyosamba ilieleza kuwa Kamati ya Sheria na Hadhi za wachezaji imeidhinisha kuwa Kakolanya ni mchezaji huru kutoka na kuidai Yanga mshahara wa miezi miwili pamoja na fedha za usajili.