Jumatatu , 18th Dec , 2017

Msanii Madee ambaye pia anafahamika kuwa mmoja wa waasisi wa kundi la muziki la Tip Top, ameamua kuongeza jeshi baada ya kuongeza wasanii ambao anawasimamia kazi zao.

Madee ambaye anajulikana kuwa msimamizi (meneja) wa Dogo Janja tangu alipokabidhiwa na marehemu baba yake, sasa hivi amemuongeza msanii anayejulikana kwa jina la Gazza, ambaye tayari ameshaachia kazi mpya aliyomshirikisha chini ya uongozi wake.

Licha ya msanii huyo kujikita kwenye kusimamia wasanii wachanga, amesema bado hajafikiria kuanzisha lebo yake kama ilivyo kwa wasanii wengine, isipokuwa ataendelea hivyo kwa sasa.

Itazame hapa chini video mpya ya Gaza Ft Madee