
Maafisa wa Uturuki wamesema washambuliaji watatu walifyatua risasi katika eneo la kuingilia uwanja huo jana na kisha kujilipua baada ya polisi kuanza kuwarushia risasi.
Waziri Mkuu Binali Yildirim amesema kuna viashiria vya awali vinavyoonyesha kuwa kundi linalojiita Dola ya Kiislam (IS) linahusika na shambulio hilo.
