Jumatatu , 28th Dec , 2015

Wakala wa mchezaji wa kimataifa Mbwana Ally Sammata, Jamal Kasongo amesema anaamini mpaka mwakani kutakuwa na wachezaji sita kutoka Tanznaia ambao watakuwa wanacheza soka la kulipwa ili kuweza kuitangaza nchi katika ramani ya soka.

Kasongo amesema, hivi sasa anafanya kazi na wachezaji mbalimbali ambao ni Farid Mussa, Hajji Mwinyi, Haruna Chanongo, Abuu Ubwa, Makame Msungu, Rajab Zahir, Salim Mbonde, Mohammed Ibrahim, Hija Mhando na John Bocco na kwa sasa wana orodha ndefu ya mawakala ambao wapo nchi za Ulaya ambao wanashirikiana ili kuhakikisha wanafikia malengo waliyojiwekea.