Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zlatan aipa ubingwa Man United kwa masharti

Jumapili , 15th Jan , 2017

Wakati United  ikijianda kuivaa Liverpool leo saa moja jioni, mshambuliaji wake mwenye maajabu Ibra Magic raia wa Sweden Zlatan Ibrahimovic amesisitiza kuwa Manchester United bado inaweza kutwaa ubingwa Ligi Kuu Uingereza msimu huu.

Zlatan Ibrahimovic

 

Man United imehaha kuendeleza kiwango bora katika hatua za awali msimu huu, lakini mashetani hao wekundu wameshinda mechi tisa mfululizo katika michuano yote, sita zikiwa ni Ligi Kuu.

Kikosi hicho cha Jose Mourinho bado kipo katika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi lakini wamepunguza pengo la pointi dhidi ya vinara Chelsea hadi kufika pointi 10 na Ibrahimovic anaamini timu yake inaweza kupambana kutwaa ubingwa wa ligi iwapo wataifunga Liverpool katika uwanja wa Old Trafford siku ya leo.

"Ligi haitabiriki. Hakuna timu ambayo unaweza kusema itashinda na ikafanya hivyo," Ibrahimovic alikiambia Sky Sports News. "Chelsea imekuwa ikifanya vizuri, wanacheza mara moja kwa wiki, wana hali nzuri na nguvu nyingi kila wanapocheza, lakini walikuwa na wakati mgumu mwanzoni lakini walizinduka.

"Kama tutapanda pale na kuwasumbua, kila timu ina kipindi chake cha mafanikio. tumekuwa na wakati mzuri, tukishinda, tukipoteza na sasa tunashinda tena. Natumai tutaendelea hivyo na tunasubiri wengine wafanye makosa.

"Jumapili ni fursa nyingine ya kuchukua pointi kutoka nne bora. Kama tunaweza kuanza vita dhidi ya timu zilizo kwenye nne bora, baada ya kupoteza pointi nyingi ambazo hatukupaswa kuzikosa. Pengo limekuwa dogo sasa, na pointi hizo tunaweza kuanza kuzichukua kwa Liverpool,"

Ibrahimovic ambaye alitua Old Trafford kwa uhamisho huru amefunga magoli 18 katika michuano yote akiwa United, ikiwa ni pamoja na magoli 13 ya ligi

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu