Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yainyuka Coastal bao 2-0 Mkwakwani

Jumapili , 16th Jan , 2022

Klabu ya Yanga imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Coastal Union, na sasa kikosi hicho cha timu ya wananchi kinaongoza Ligi kwa tofauti ya alama 8. Huu ni ushindi wa kwanza kwa Yanga mkoani Tanga baada ya miaka 6.

Saidi Ntibazonkiza akishangilia baada ya kufunga bao la pili

Mabao ya Yanga kwenye ushindi huo wa mabao mawili yamefungwa na Fiston Mayele aliyefunga bao la kwanza dakika ya 41 na bao la pili limefungwa na Saidi Ntibazonkiza dakika ya 90. Kwa ushindi huu Yanga inafikisha alama 32.

Huu ni ushindi wa 5 ugenini kwa Yanga msimu huu wa 2021-22 katika michezo 7 waliocheza ugenini wakiwa wametoka sare michezo 2, wamevuna alama 17 katika michezo hiyo ya ugenini, lakini pia Yanga wameshinda kwa mara ya kwanza katika dimba la Mkwakwani tangu mwaka 2015 ambapo walishinda bao 1-0.

Yanga wanasalia kileleni mwa msimamo na sasa wanaongoza Ligi kwa tofauti ya alama 8 dhidi ya Simba wenye alama 24 wakiwa nafasi ya pili lakini Simba wamecheza michezo 10 huku yanga wameshacheza michezo 12.

Mchezo mwingine wa Ligi leo umechezwa huko mkaoni Rulwa ambapo Tanzania Prisons waliwa wenyeji wa KMC FC na mchezo huo umemalizika kwa KMC kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 mabao ya Kelvin Kijiri na Ally Ramadhani.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu