Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga wanaongoza kwa 'kuua' watu - JB

Jumatano , 29th Mar , 2017

Msanii Jacob Stephen maarufu kama JB amefunguka na kusema klabu ya Yanga ni chanzo cha watu wengi kupatwa na matatizo ya moyo ambayo hupelekea vifo kwa sababu klabu hiyo haina furaha wala haiwapi furaha mashabiki wake ukifananisha na klabu ya Simba.

JB

JB alisema hayo kupitia katika kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa kupitia ukurasa wa facebook wa EATV na kusema toka ameifahamu Simba akiwa mtoto mdogo imekuwa ni klabu ambayo inampa furaha muda mwingi.

Amesema timu ya Yanga haiwezi kuwa ya kimataifa kutokana na historia yake ya michezo inayoonesha kutolewa katika baadhi ya mashindano ya kimataifa mara kwa mara.

"Watani zetu wa jadi wanaongoza kwa kuua watu maana wanafungwa kila mara ila mimi binafsi huwa nafurahi sana nikiona wanafungwa na hata kama nikiwa kwenye hasira zangu, mke wangu akija akinionesha video zinaonesha wanavyofungwa huwa 'automatical' nacheka". Alisema JB

Akizungumzia chimbuko la yeye kuanza kushabikia Simba, JB anasema

"Mimi kushabikia Simba ni kama nimerithishwa na baba yangu, nakumbuka wakati nipo mdogo tulikwenda uwanjani na siku hiyo Simba ilishinda bao 6, nikajikuta naipenda ile timu na nilipomwambia baba yangu aliniambia ukitaka furaha siku zote kuwa Simba. Yanga ni klabu kubwa Afrika na imebahatika kuchukua ubingwa mara kadhaa, ila aina ya mpira wa Yanga hainifurahishi ila ni klabu ambayo imesababisha watu wengi kupata magonjwa ya moyo, hivyo Yanga hakuna furaha" alisema JB 

Kichuya

JB anasema kama mwaka huu Simba haitachukua ubingwa yeye ataumia sana na kulia kabisa 

"Kiukweli Kichuya aliniliza kwa furaha maana goli aliloifunga Yanga siku zile lilikuwa ni goli la ajabu sana, sikutegemea kabisaa kupata goli tukiwa 10 uwanjani hivyo siku zile nililia kwa furaha. Lakini pia wachezaji wananifahamu vizuri wasipofanya vizuri huwa nawapigia simu nawatukana sana tu, maana namba za wachezaji wote wa Simba ninazo hivyo wananijua" alisema JB 

Mbali na hilo JB anadai katika vitu ambavyo huwa vinamfurahisha sana katika maisha yake ni kumfunga Yanga tena wakati timu yake Simba ikiwa pungufu uwanjani.

"Vipo vitu vitatu ambavyo mimi napenda moja ni kwenda mbinguni, mbili ni kuishi maisha matakatifu na cha tatu ni kumfunga Yanga ni kitu ambacho napenda sana kuna muda mwingine naweza kuboreka lakini nikiangalia magoli ya Kichuya nabaki na tabasamu. Hata mke wangu analijua hilo saizi akiona nimenuna tu anaweka yale magoli yaani najikuta na furaha ya ajabu na kuanza kutabasamu" alisisitiza JB 

Vile vile JB amesema katika wachezaji wote wa kikosi cha Yanga anampenda zaidi Saimo Msuva kwa kuwa anaujua vizuri mpira na kumshauri ajiunge na Simba ili aweze kupata furaha ya moyo wake.

Msuva

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto