Jumatatu , 31st Mar , 2014

Chama cha Mchezo wa Table Tenis TTTA,kimepata udhamini wa wachezaji wanne wa mchezo huo na kocha mmoja kutoka serikalini, kuelekea nchini China kujiandaa na Michuano ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika jijini Grascow Scotland, julai mwaka huu.

Akiongea na Michezo ya East Africa Radio,Mwenyekiti wa kamati ya ufundi na mashindano ya TTTA,Yahaya Mungirwa amesema tayari wameshapeleka majina hayo katika kamati ya Olimpiki Tanzania TOC kwa uhakiki,tayari kuelekea nchini humo kwa maandalizi

Mungirwa amesema fursa hiyo ni muhimu kwa wachezaji wa mchezo huo kwani watapata uzoefu kutoka nchini China kutokana na nchi hiyo kuwa na kiwango cha kimataifa katika mchezo wa table tenis.