Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wasiotaka kucheza Arsenal wabaki nyumbani- Xhaka

Jumanne , 17th Mei , 2022

Nahodha wa klabu ya Arsenal Granit Xhaka amewajia juu wachezaji wa kikosi hicho baada ya kufungwa na Newcastle United mabao 2-0 kwenye mchezo wa Ligi Kuu England. Akiwataka wachezaji ambao hawapo tayari kujitoa kuipambania klabu wabaki nyumbani au wasicheze kabisa.

Arsenal wamefungwa michezo miwili mfululizo na kupoteza matumaini ya kucheza Ligi ya mabingwa msimu ujao

Xhaka hajapendendwa na kiwango cha uchezaji kilichoonyeshwa na baadhi ya wachezaji wenzake kwenye mchezo huo ambao ulikuwa ni muhimu kwao kushinda ili kufufua matumaini yakufuzu Ligi ya mabingwa Barani ulaya kwa mara ya kwanza baada ya misimu 5.

"Kama mtu hayuko tayari kucheza mchezo huu, akae nyumbani, haijalishi umri wako. Ukiwa na woga, kaa benchi au ubaki nyumbani, unahitaji watu waje kucheza mpira. Ni moja ya michezo muhimu sana kwetu. Tumewaangusha sana watu waliokuja hapa. Amesema Xhaka

Kipigo hicho kimeiweka The Gunnars kwenye mazingira magumu ya kufuzu kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao kutoka na kipigo hicho ambacho kimewafanya wasalie nafasi ya 5 kwenye msimamo wa EPL wakiwa na alama 66 tofauti ya alama 2 dhidi ya Tottenham wenye alama 68 wakiwa nafasi ya 4 na umebaki mchezo mmoja kabla ya Ligi kumalizika.

Kwa matokeo hayo ili Arsenal iweze kufuzu kucheza Champions league msimu ujao inabidi washinde mchezo wao wa mwisho wa ligi dhidi ya Everton lakini pia Tottenham wafungwe na Norwich City ili wao waweze kumaliza katika nafasi ya 4. Katika ushindi huo wa Newcastle bao la kwanza beki wa Arsenal Ben White alijifunga na Bruno Guimares alifunga bao la Pili.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu