Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waamuzi wapo tayari kutenda haki

Jumanne , 7th Aug , 2018

Kuelekea mchezo wa kesho Jumatano Agosti 11 wa game 3 ya 'best of three' nusu fainali ya michuano ya Kikapu ya Sprite Bball Kings kati ya Portland dhidi ya Mchenga Bball Stars, Kamishna wa ufundi wa TBF Manase Zabroni amesema waamuzi wamejipanga kuhakikisha haki inatendeka.

Waamuzi wa Kikapu wakiongozwa na Manase Zabroni (kulia).

''Kama tulivyoanza mwanzo wa mashindano kumekuwa hakuna lawama kuhusu waamuzi hivyo tutamaliza nusu fainali kesho kwa mwendo huo na mshindi atapatikana kwa haki na atakwenda kucheza fainali na wenzao wa Flying Dribblers ambao nao wamefika hatua hiyo bila malalamiko kwa waamuzi'' - amesema.

Mchezo wa kesho utazikutanisha timu za Portland dhidi ya Mabingwa watetezi wa michuano hiyo inayoandaliwa na East Africa Television LTD na kudhaminiwa na kinywaji cha Sprite, Mchenga Bball Stars. Mchezo huo ambao umekuja baada ya timu hizo kushinda mechi moja kila timu kwenye game 1 na game 2, utapigwa kwenye viwanja Don Bosco Oysterbay.

Mchenga Bball Stars (nyeupe) na Portland (kijani) kweye mechi ya game 2.

Portland walitoka nyuma kwa kupoteza game 1 kwa pointi 70 kwa 54 kabla ya kusawazisha game 2 kwa kushinda pointi 71 kwa 64. Game 3 itakuwa na ushindani mkubwa hususani kwa vinara wa pointi katika timu hiyo ambao ni Denis Babu kwa Portland mwenye pointi 104 kwenye mechi 5 na Baraka Sadick wa Mchenga mwenye pointi 64 katika mechi 4.

Mechi hiyo itakayotoa tiketi ya kwenda kucheza fainali na Flying Dribblers kuwania milioni 10 kwa bingwa, milioni 3 kwa timu itakayoshika nafasi ya pili na milioni 2 kwa MVP itaanza majira ya saa 10:00 jioni.
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu