
Beki wa kulia wa Yanga, Hassan Kessy
Mwambusi amesema, wamewachukua wachezaji hao sio kwa kuwatumia leo au kesho bali ni kwamuda mrefu kwani bado umri wao unaruhusu na pia wanavipaji.
Mwambusi amesema, wachezaji hao pia wanatakiwa kupata uzoefu na wachezaji waliowakuta ili kuweza kupata namba katika kikosi.
Mwambusi amesema, kwa sasa wanaendelea na harakati za kuweza kuwasajili katika shirikisho la Soka barani Afrika CAF.
Mpaka sasa Yanga imefanikiwa kuwasajili wachezaji wanne ambaye ni Hassan Kessy kutoka Simba, Vicent Andrew"Dante" kutoka Mtibwa Sugar, Juma Mahadhi kutoka Coastal Union na mlinda mlango Beno Kakolanya kutoka Tanzania Prisons ambaye bado hajaungana na kikosi kwa ajili ya mazoezi.