Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tetesi za usajili Ulaya, Neymar Jr awekwa sokoni

Alhamisi , 23rd Jun , 2022

Taarifa za usajili barani Ulaya leo Alhamisi Juni 23, 2022. Miongoni mwa taarifa Ousmane Dembela anataka kubaki Barcelona, PSG wanampango wakumfuta kazi Pochettino na Neymar huwenda akuuzwa ikija offa nzuri.

Neymar Jr ana umri wa miaka 30

Winga wa FC Barcelona Ousmane Dembele amemwambia kocha mkuu wa klabu hiyo Xavi Hernandez kuwa anataka kubaki Barcelona. Mkataba wa Dembele na Barcelona unamalizika mwishoni mwa mwezi huu Juni 2022. Winga huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 25 anahusishwa kujiunga na Chelsea ya England. Kama hata ongeza mkataba mpya ataondoka akiwa mchezaji huru.

kocha wa Nice Christopher Galtier amefikia makubaliano ya kujiunga na klabu ya PSG kwa mkataba wa miaka miwili (2). Kwa mujibu wa ripoti kutoka nchini Ufaransa zinaripoti kuwa kocha Galtier amefikia makubaliano na viongozi wa PSG kuja kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo akichukua mikoba ya Mauricio Pochettino anayetarajiwa kufutwa kazi.

Rais wa PSG Nasser Al-Khelaifi alidhibitisha kuwa wapo kwenye mazungumzo na kocha huyo. PSG inampango wa kumfuta kazi Pochettino baada ya kushindwa kukiongoza kikosi hicho kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa barani ulaya baada ya kutolewa na Real Madrid raundi ya 16 bora.

Manchester United wapo tayari kumuuza mshambuliaji wao Anthony Martial kwa ada ya uhamisho ya pauni miliioni 20 ambayo ni zaidi ya Bilioni 57 kwa pesa ya Tanzania. Martial ana mkataba wa miaka miwili (2) na Manchester United. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa ufaransa hajawa na kiwango bora kwani katika misimu miwili iliyopita amefunga mabao 9 tu kweye michezo 59.

Mabingwa wa Ufaransa klabu ya PSG wapo tayari kumuuza nyota wake Neymar Jr katika dirisha hili la usajili la majira ya joto kama watapata offa nzuri hii ni kwa mujibu wa taarifa kutoka nchini Hispania. Kwa sasa PSG wanataka wachezaji vijana zaidi na Neymar mwenye umri wa miaka 30 hawamatazami tena kama mchezaji anayeweza kuwapa mahitaji yao kwa sasa.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali